Swahili
Surah Al-Qalam ( The Pen ) - Aya count 52
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
( 1 ) 
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ
( 2 ) 
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ
( 3 ) 
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ
( 4 ) 
Na hakika wewe una tabia tukufu.
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
( 5 ) 
Karibu utaona, na wao wataona,
بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ
( 6 ) 
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ
( 7 ) 
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ
( 8 ) 
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
( 9 ) 
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ
( 10 ) 
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ
( 11 ) 
Mtapitapi, apitaye akifitini,
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
( 12 ) 
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
( 13 ) 
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ
( 14 ) 
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
( 15 ) 
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ
( 16 ) 
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
( 17 ) 
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
( 18 ) 
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ
( 19 ) 
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ
( 20 ) 
Likawa kama usiku wa giza.
فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ
( 21 ) 
Asubuhi wakaitana.
أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ
( 22 ) 
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ
( 23 ) 
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ
( 24 ) 
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ
( 25 ) 
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ
( 26 ) 
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
( 27 ) 
Bali tumenyimwa!
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
( 28 ) 
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
( 29 ) 
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ
( 30 ) 
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ
( 31 ) 
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ
( 32 ) 
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
( 33 ) 
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ
( 34 ) 
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ
( 35 ) 
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
( 36 ) 
Mna nini? Mnahukumu vipi?
أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ
( 37 ) 
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
( 38 ) 
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
( 39 ) 
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
( 40 ) 
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ
( 41 ) 
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
( 42 ) 
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ
( 43 ) 
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا الْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ
( 44 ) 
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
وَأُمْلِي لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ
( 45 ) 
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
( 46 ) 
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
( 47 ) 
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ
( 48 ) 
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ
( 49 ) 
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ
( 50 ) 
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ
( 51 ) 
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
( 52 ) 
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.