Swahili
Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out ) - Aya count 46
وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا
( 1 ) 
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَالنَّاشِطَاتِ نَشْطًا
( 2 ) 
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَالسَّابِحَاتِ سَبْحًا
( 3 ) 
Na wanao ogelea,
فَالسَّابِقَاتِ سَبْقًا
( 4 ) 
Wakishindana mbio,
فَالْمُدَبِّرَاتِ أَمْرًا
( 5 ) 
Wakidabiri mambo.
يَوْمَ تَرْجُفُ الرَّاجِفَةُ
( 6 ) 
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتْبَعُهَا الرَّادِفَةُ
( 7 ) 
Kifuate cha kufuatia.
قُلُوبٌ يَوْمَئِذٍ وَاجِفَةٌ
( 8 ) 
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبْصَارُهَا خَاشِعَةٌ
( 9 ) 
Macho yatainama chini.
يَقُولُونَ أَإِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِي الْحَافِرَةِ
( 10 ) 
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَإِذَا كُنَّا عِظَامًا نَّخِرَةً
( 11 ) 
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُوا تِلْكَ إِذًا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌ
( 12 ) 
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ
( 13 ) 
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِالسَّاهِرَةِ
( 14 ) 
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ مُوسَىٰ
( 15 ) 
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذْ نَادَاهُ رَبُّهُ بِالْوَادِ الْمُقَدَّسِ طُوًى
( 16 ) 
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
اذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُ طَغَىٰ
( 17 ) 
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰ أَن تَزَكَّىٰ
( 18 ) 
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
( 19 ) 
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَاهُ الْآيَةَ الْكُبْرَىٰ
( 20 ) 
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
( 21 ) 
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ
( 22 ) 
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
( 23 ) 
Akakusanya watu akanadi.
فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ
( 24 ) 
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
فَأَخَذَهُ اللَّهُ نَكَالَ الْآخِرَةِ وَالْأُولَىٰ
( 25 ) 
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِّمَن يَخْشَىٰ
( 26 ) 
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
أَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ السَّمَاءُ ۚ بَنَاهَا
( 27 ) 
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّاهَا
( 28 ) 
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَاهَا
( 29 ) 
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
وَالْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَاهَا
( 30 ) 
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
أَخْرَجَ مِنْهَا مَاءَهَا وَمَرْعَاهَا
( 31 ) 
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
وَالْجِبَالَ أَرْسَاهَا
( 32 ) 
Na milima akaisimamisha,
مَتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ
( 33 ) 
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَاءَتِ الطَّامَّةُ الْكُبْرَىٰ
( 34 ) 
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ مَا سَعَىٰ
( 35 ) 
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
( 36 ) 
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
( 37 ) 
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
وَآثَرَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا
( 38 ) 
Na akakhiari maisha ya dunia,
فَإِنَّ الْجَحِيمَ هِيَ الْمَأْوَىٰ
( 39 ) 
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ وَنَهَى النَّفْسَ عَنِ الْهَوَىٰ
( 40 ) 
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
فَإِنَّ الْجَنَّةَ هِيَ الْمَأْوَىٰ
( 41 ) 
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا
( 42 ) 
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا
( 43 ) 
Una nini wewe hata uitaje?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَاهَا
( 44 ) 
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
إِنَّمَا أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَاهَا
( 45 ) 
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَاهَا
( 46 ) 
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.